Tuesday, August 31, 2010

JAMANI DUH!!!

Jamaa kauchuna lakini mkewe akamkoleza kwa kicheko!!!!
Mwenyewe akachekelea ndoa taamu!!
Watu wakapiga msosi!
Wakampongeza na kutoa zawadi!
Aaaah brother Mashaka nae akapata nafasi ya kukoleza ndoa yake hii ni siku Hansen Fandey alipomchukua Susan kuwa mkewe mjini Morogoro, ilikuwa taaaamu sana!!!!




Monday, August 30, 2010

UCHAGUZI 2010

Chadema
CCM
CUF
Inakuwa raha sana kipindi hiki cha kampeni kwani kwenye viwanja utakuta watu kibaaao katika karibu kila mkutano wa vyama vikubwa lakini matokeo hayaendani na mikutano. Tunasubiri tuone mwisho baada ya uchakachuaji!!!!

Friday, August 27, 2010

MSAADA KWA YATIMA

Osman Kazi akizungumza katika hoteli ya Movernpick Royal Palm leo asubuhi.
Meneja wa Operations wa Movernpick akizungumzia msaada wa hoteli yake.

Baadhi ya walezi wa yatima waliokuwepo katika mkutano huo wakisikkiliza mpango mzima.


Mkurugenzi wa PSET, Osman Kazi akizungumzia bonanza ambalo amaenadaa kwa mara ya kwanza kwa ajili ya watoto yatima siku ya Idd pili katika viwanja vya leaders Club, Kinondoni jijini Dar es Salaam. Watoto wanaoishi katika mazingira magumu wataandaliwa michezo na burudani mbalimbali ikiwa ni pamoja na chakula na vinywaji.Kushoto kwake ni Bi Mwanaisha Magambo wa New Life Orphanage. Kulia ni Mwakilishi wa Royal Palm Seraphin Lusala.

Kazi ameomba wadau wenye moyo mwema na walio na haja ya kuchangia watoto hao wajitolee kwa vitu mbalimbali vinavyoweza kufanikisha siku hiyo ikiwa ni pamoja na uandaaji ambako vinahitajika vyakula, vinywaji vitamu, vifaa vya michezo na hata fedha ili kufanikisha.

Kikubwa ni watu kujitokeza na kujumuika na watoto hao pamoja na familia zao katika siku ya tukio ili kuifanya iwe ya mafanikio zaidi. Hotel Movenpick Royal Palm imejitolea uku,nbi wa mikutano na vinywaji kwa jili ya maandalizi.

Kwa mawasiliano piga simu namba 0713 477300 ama 0715 732333.

PAMOJA TUNAWEZA, INSHAALLAH!!!

Thursday, August 26, 2010

KAMPENI ZA KIKWETE NGARA


Mkutano wa kampeni kwa mgombea wa CCM uliokuwa ufanyike mjini Ngara jana jioni ulilazimika kuahirishwa baada ya helkopta aliyokuwa akitumia kushindwa kumpeleka mjini humo kutokana na hali mbaya ya hewa.
Hata hivyo ilimlazimu Rais Kikwete kutumia barabara ambapo aliwasiri mjini humo usiku jkwajili ya kuongea na wananchi, hivyo mkutano huo umeahirishwa hadi leo mapema asubuhi.
Wananchi waliofurika katika viwanja vya posta ya zamani kwa ajili yasikiliza hotuba hiyo, waliambiwana Mwenyekiti wa CCM Hellen Adrian, baadae jana saa 11 jioni kuwa mkutano huo usingekuwepo hadi leo.
Baadae usiku Rais aliwasiri kwas njia ya barabara na kuandaliwa futari na kinamama wa wilayani humo kama inavyoonekana alipopokelewa kwa jili ya masafa zaidi kwajili ya kampeni.

Mdau Yusuf Mwenda (Juu) akiweka mikakati ya kampeni akiwa mgopmbea wa udiwani kata ya mikochweni huku diwani aliyemaliza muda wake Anold Maruma akimwekea msisitizo kwa wanachama wa CCM Kata hiyo. Mtanange unaendelea na watu wanaungana mkono. Buig UP!!!!

Wednesday, August 25, 2010

BANGO LA SLAA LATOKA

Haya wakati kampeni za Chadema zinakaribia bango hili limeandaliw akumnadi mgombea!

Tuesday, August 24, 2010

USALAMA WA RAIA

Vijana wa kamanda Tossi (FFU) wakiwa katika mavazi ya kisasa ya kufanyizia
wanaojifanya wajanja wakati wa uachaguzi. Mtakoma mwaka huu, mpambano wa mawe kama Tarime mwisho!!

Friday, August 13, 2010

UCHAKACHUAJI





Dodoma:Kamati Kuu ya CCM sasa inakutana ili kukamilisha zoezi la kuchakachua waliochakachua wenzao na kutuletea wagombea rasmi!!!!

JIJINI MWANZA

Utaipenda!

HATA MIMI?

Sijui ni kupongezana ama?

KONYAGO WAZINDUA KINYWAJI KIPYA

Kampuni ya tanzania Distilleries Ltd imezindua kinywaji kipya chenye ladha ya nanasi kiitwacho Bismark Rocks ambacho kwa sasa ni mahsusi kwa walevi wa Kanda ya ziwa sijui wa Dar tutapata lini hii kitu?
Meneja Masoko wa TDL, Joseph Chibehe akizungumza wakati wa kuzindua kinywaji hicho.

Mikono juuu!!!
Meneja mauzio wa TDL Kanda ya Ziwa Dilley Bhanji akionyesha katoni ya viroba vya kinywaji hicho.

Inatamaniwa mpaka na mademu, kudadadadeki!!!!!
Mzee wa Sumo sasa nimeamua kujitosa kugombea Uenyekiti wa Chama cha waandishi wa habari za Michezo napambana na vigogo wa kutisha lakini naamini nitawagalagaza! Yupo Juma Pinto, na Masoud Sanani!!!! Inshallah!

Monday, August 09, 2010

TAMASHA LA SIMBA









Ingawa naipenda Yanga lakini.....

Nimeona nikuletee picha za Simba day kama utapata nafasi basi uweke kwenye blog wadau nao waone,ilikuwaje siku hiyo namba na ,maelezo yake ni kama ifatavyo.

Mgeni rasmi wa siku hiyo,Mh, Shamhuna,akiizindua rasmi jezi ya Simba ya ugenini na nyumbani.

Mdau akiuza jezi za Simba siku hiyo,sijui kama Simba wenyewe wanafaidika na mauzo hayo au baadhi tu ya wajanja wanajipatia hela kupitia mgongo wa klabu.

Magari ya watu mbalimbali waliohudhuria.
Twanga pepeta wakinogesha siku hiyo.

Kibonde aliyekua MC wa suku hiyo,akiyarudi magoma ya Twanga Pepeta

MDAU

JOSAA

HII NI KAMPENI

Mtu wa Chadema akiwa amevalia T shirt yenye maneno 'SIHITAJI KURA ZA WAFANYAKAZI' huku ikiwa na picha ya Mgombea wa CCM, JAkaya Kikwete. Naibu Mkuu wa Kitengo chas Propaganda CCM, Tamwe Hiza anasema si kweli kwamba Kikwete alikataa kura za wafanyakazi. Mi simo!!!

Friday, August 06, 2010

FUNDI CHEREHANI

Yaani mchina kaharibu ajira za watu zamani kila mtaa ulikuwa na fundi cherehani kwa ajili ya kuweka viraka sasahivi hakuna mwenye hamu ya hata ya kushiona kaunda suti zinatoka Beijing!

BONANZA LA MIAKA 10 YA MWANANCHI

Vijana wa The Citizen wakipasha moto kabla ya kukabiliana na wenzao wa Mwananchi.
Ukaanza mpambano wa Vuvuzelaz kelele ilikuwa kama Woza!

Nikajitahidi lakini madogo walikomaa!




Nikapewa eti redcard kwamba sijui kupuliza Vuvuzela!




Nikamuingiza Junior akatinga fainali, sasa kama sijui nani amemfanya diogo agonge kama mimi?






Wengine walizidiwa wakafaint, kidogo afe!





wengine walikimbilia kwenye menu na watoto yatima waliotujoin kutoka kuituo cha Yatiam Trust Group cha Chamazi.




Watoto yatima walijienjoy vilivyo!








Thursday, August 05, 2010

BABA NA MAMA

ALIYEKUWA mgombea wa Ubunge wa jimbo la Hanang,kupitia CCM, Rose Kamili leo anatarajia kurejesha kadi ya CCM na kujiunga na chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) wilayani Hanang mkoani Manyara.

Kamili ambaye ni Diwani wa CCM tangu mwaka 1994 katika kata ya Basotu, alitangaza uamuzi huo, juzi mara baada ya kutangazwa matokeo ya Ubunge ambapo, yalionesha ameshindwa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Mary Nagu.

Kamili ambaye ni mke wa Dk Slaa, mgombea wa Urais wa Chadema mwaka huu, alisema ameamua kujiondoa CCM kutokana na kutoridhishwa na mwenendo ya chama hicho hasa katika kampeni za ubunge.

"napenda kutangaza wazi kuwa mimi siwezi kumuunga mkono Nagu katika kampeni za ubunge na natarajia kurejesha kadi ya CCM kesho(leo)"alisema Kamili.

Kamili alisema ameamua kujiondoa CCM kutokaa na kutoridhishwa na uchaguzi huo, hasa kutokana na kitendo cha Katibu wa CCM wa wilaya hiyo, Michael Sakra kupiga kampeni wilaya nzima ashindwe.

"katibu amekuwa akiwaita viongozi wote wa CCM na kuwaagiza kuhakikisha Nagu anashinda wametumia fedha na hila nyingi hivyo nimeona basi mchango ambao nimeutoa CCM kwa zaidi a miaka 20 unatosha"alisema Kamili

Hata hivyo, alisema uamuzi wa kugombea ubunge au kutogombea atautangaza lakini anaimani chadema ina mgombea mwingine mzuri katika jimbo hilo.

Uamuzi wa kamili kujiunga na chadema utakuwa ni pigo kubwa kwa CCM Hanang na hasa kutokana na nguvu kubwa aliyokuwa nayo katika wilaya hiyo.


KATIBA KENYA

Vinara wa NDIO washerekea ushindi Kenya!Saa kumi na mbili baada ya wakenya kumaliza kupiga kura ili kupinga ama kukubali katiba mpya, matokeo yametoka na kuonyesha kuwa wengi wameikubali. Katika kura zilizopigwa NDIO wamepata 4,141,521 (asilimia 67) wakati waliopinga wamepata 2,054,946 (Asilimia 33).

Sasa kwa katiba mpya Kenya itajulikana lama Federal Republic of Kenya.

DR SLAA SONGEA

MGOMBEA Urais kwa tiketi ya Chadema, Dk. Willbrod Slaa, jana alipanda jukwaani saa 12.04 na kumaliza saa 12.30 jioni, huku akieleza kuwa kuchelewa kwake kumetokana na Helkopta yake kupata hitilafu akitokea mjini Songea, hali iliyomlazimu kukodi ndege ya dharura ili aweze kuwafikia wananchi hao waliokuwa wakimsubiri tangu saa 9 mchana.

Alisema umasikini wa wakazi wa mikoa ya kusini, Lindi, Mtwara na Ruvuma unatokana na wakazi hao kuikumbatia CCM, na kwamba ni wajibu wao kupima hali zao za maisha miaka 40 tangu Tanzania ipate uhuru huku CCM kikiwa chama pekee kilichotawala.

“CCM ndiyo iliyowafikisha hapo mlipo, miaka 40 tangu uhuru bado hali ya maisha ya watu wa kusini ni duni, barabara ni moja tu ya lami, ukiacha hiyo utang’atwa na nyoka maporini” alibeza mgombea huyo.

Baadhi ya wasikilizaji wakiongea na mwandishi wa habari hizi walimsifu Dk. Slaa kwa hotuba yake ya ushawishi, huku wengine wakimdhihaki kwa madai kuwa pweza aliyeitabiria Hispania kutwaa kombe la dunia pia amemtabiria Dk. Slaa kuwa rais.

“Dk. Slaa kwangu namuona ni mtu anayekerwa na matatizo ya watanzania maana hata hotuba yake imeweka wazi na kuchambua matatizo yetu……pweza amemtabiria kuwa rais” alisema Joshua George


Wednesday, August 04, 2010

MATOKEO






WAKATI Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Chilonwa, Dodoma, kikithibitisha matokeo ya kura za maoni kwa Mtera ambako mwanasiasa mkongwe, John Malecela ameshindwa na kukubali matokeo, baadhi ya wagombea walioshindwa wakiwamo mawaziri, wamelalamikia matokeo.

Jana asubuhi kulikuwa na taarifa za kutolewa kwa matokeo ya Mtera, huku habari zikidai kuwa Mzee Malecela alikuwa ameshinda, lakini matokeo hayo rasmi ya CCM Chilonwa, yalithibitisha kuwa Livingstone Lusinde alikuwa amembwaga kiongozi huyo wa siku nyingi.
Endelea

Tuesday, August 03, 2010

UCHAGUZI 2010


Kwa kujua matokeo ya awali na wagombea waliostaafishwa kwa ridhaa ya umma angalia hapa