Sunday, October 19, 2008

JAMANI MTOTO


Yaani huwa inaniuma sana ukatili unaofanywa na wabongo, imagine katoto kazuri kama haka kenye furaha hakajui watu wanavyotafuta maalbino kwa ajili ya ushenzi wao. Kikubwa nilichogundua ni kuwa albino si lazima azaliwe na albino, mcheki mama yake! (What a motherly smile!)

6 comments:

Anonymous said...

ooooooooooooh mtoto mzuri na mama ni mrembo, this is a lovely photograph. Such happiness and joy!

Anonymous said...

HIYO PICHA ISA WA MICHUZI KAIONA NADHANI ATAKOMA KUJIDAI AKIIONA PICHA IMETULIA

Unknown said...

Hujafa, hujaumbika

Anonymous said...

Rafiki zangu,
mnakumbuka zama zile tukienda Ocean Road Hospitali kuangalia sinema za James Bond (Live and Let Die) kwa ndugu zetu hawa?
Mnamkumbuka kiongozi wa hawa ndugu zetu Mzee Lameck?
Mnakumbuka tukijifunza kuvuta sigara pale kwenye kioski cha kibaiskeli nje ya vyumba vya kujifungulia kina mama? Mnakumbuka wale wazazi waliokuwa wanasaidiwa kujifungua na mama zetu barabarani Mtaa wa Luthuli?
Mnakumbuka vilio na kelele na za kina mama zetu wakati wa kujifungua?
Mnawakumbuka dada zetu mapacha tuliosoma nao Forodhani Sekondari na kusali nao kanisa la Mtakatifu Josefu?
Quo Vidas Tanzania? = Tanzania unaenda wapi?

Haven´t we learn from Mauaji ya Shinyanga? Mauaji na mateso ya kina Twiga Nindwa na Mazenghenhuka? Mauaji na mateso yaliowapeleka mahakamani na wauaji? Yaliowapeleka mahakamani na kuwafunga na kuwalazimisha kujiuzuru viongozi, mawaziri, mapolisi na maofisa upelelezi?

Kama historia haitukumbushi na kutufunza, nini kitatukumbusha na na kutufunza? Turejee ya Shinyanga ili yatupe njia mkabala ya kukabiliana na haya ya sasa. Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema na Upendo tuongoze katika njia zako. Amen.

Anonymous said...

Bro, asante sana picha nzuri sana.

Mitsuka Magnolia S said...

Jamani nakaomba mie hako katoto..
That's a one proud mama yaani wamependeza sana..