Friday, January 14, 2011

MZEE ALONGA

WAZIRI Mkuu Mstaafu Cleopa Msuya amezungumzia sakata la Kampuni ya Kufua Umeme wa Dharura ya Dowans akieleza kuwa mpaka sasa hafahamu kwa nini Tanzania inapaswa kuilipa fidia kampuni hiyo ya kigeni inayodaiwa kuingia nchini kitapeli.

Akizungumza nyumbani kwake Upanga jijini Dar es Salaam, Msuya alisema anaamini hata Watanzania wengine, watakuwa wanajiuliza swali hilo.

"Wakati mwingine nashindwa hata kuzungumzia suala hili kwa sababu hadi sasa, sijui Dowans wanapaswa kulipwa kwanini. Naaamini si mimi tu ninayejiuliza swali hili, hata Watanzania wengine wengi hawajui kwanini Serikali inapaswa kuilipa Dowans," alisema Msuya. Endelea


No comments: