Wednesday, September 10, 2008

BONGO MUSIK

Muziki wa Kibongo wawapaigaisha watu Ng'ambo!
Ni juzi tu siku ya jumamosi ya tarehe 09/08/2008 katika viwanja vya Robstock Park,katikati ya mji wenye maghorofa marefu FRANKFURT City,Ujerumani,
Bendi maarufu ya mziki wa dansi barani ulaya The Ngoma Africa Band inayoongozwa
na mwanamziki nyota mahiri Ebrahim Makunja alimaarufu Ras Makunja na mdundo wao
wa dansi la Tanzania ambao umekuwa maarufu kwa jina la bongo dansi ulifanikiwa tena kwa mara nyingine kuyatingisha maghorofa marefu za mji huo na kuwatia kiwewe maelfu ya washabiki walio udhuria katika maonyesho hayo!
Kabla ya bendi ya Ngoma Africa kupanda jukwaani onyesho lilikuwa limetulia (cool) huku bendi nyingine kutoka Oteng Band (Ghana) hilikuwa ikitumbuiza,baada ya moja ya watayarishaji kuwatangazia washabiki kuwa sasa inapanda jukwaani bendi maarafu ya
The Ngoma Africa band(Tanzania) hapo tena kukawa hakuna mshabiki aleyakaa chini,
si wazungu ! wala si weusi,watoto kwa wakubwa palikuwa kama vile uwanja uliovamiwa na
siafu!
Ras Makunja mwenyewe akikiongoya jukwaani kikosi hiko chenye utajili wa wanamziki
wenze kujua kuporomosha mziki unao chezeka na kudatisha washabiki hakili
kwa mdundo wao wa nzimbo ya kiswahili!
Mlindimo wa mdundo huo haukumuacha mtu uliwachanganya hakili washabiki na kujisahau kabisa kuwa ni raia wa nchi,dini,rangi mbali mbali!
Ni Mziki pekee wa dansi wa Tanzania unaofanikiwa kuzoa mashabiki kwa kasi kubwa barani ulaya !na kuziacha hoi baadhi ya bendi yingine wakiwa na halama ya mshangao!
kwa jinsi gani!? washabiki wanatiwa kiwewe na mdundo huo wa Ngoma Africa Band,
Mpiga solo Gitaa wa bendi hiyo Christian Bakotessa a.k.a ChrisB ,aliwachengua washabiki na mlio wa gitaa la solo! mara tu pale aliporushwa hewani kwa kuitwa jina lake !na Ras makunja basi mlio wa gitaa hilo ni kazi moja tu!
Katika onyesho hilo pia kulikuwako wanahabari kutoka RADIO DEUTCHE WELLE wakiongozwa na mtangazaji mashuhuri wa Idhaa ya Kiswahili Bi.Swaum Mwasimba !
The Ngoma Africa Band itapanda tena jukwaani katika onyesho lingine kubwa la
AFRIKA FESTIVAL siku ya 29/08/2008 katikati mji wa Hamburg,katika jukwaa la wazi
la Hamburg-Altona ambako nako washabiki wanawasubiri kwa hamu.
Siku ya 30/08/2008 Ngoma Africa wamehalikwa kutumbuiza katika maonyesho ya Utamaduni wa Afrika (AFRIKA FEST) yatakayo fanyika katika mji wa Krefeld nako huko
kutakuwa na vunja jungu la PATA SHIKA ! za NGUO KUCHANIKA

No comments: