Tuesday, March 10, 2009

MWINYI

Mzee Ali Hassan Mwinyi akijadiliana jambo na Sheikh Mkuu wa mkoa wa dar es Salaam katika Baraza la Maulid leo jioni.
Mzee Mwinyi akihutubi abaraza la Maulid leo kabla ya kunaswa kibao na muunini wa kiislamu ambaye hakujali umri wakla heshima kw amzee wetu!!!!

RAIS Mstaafu wa Awamu ya Pili, Alhaj Ali Hassan Mwinyi, leo jioni amejikuta katika wakati mgumu baada ya kijana Ibrahim Said kuvamia jukwaa alipokuwa na kumzaba kibao shavuni.
Tukio hilo ambalo halikutarajiwa lilitokea jana majira ya saa 12:20 hivi wakati rais huyo mstaafu alipokuwa akihutubia Baraza la Maulid kuadhimisha kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (SAW) lililohudhuriwa na Waislam wengi katika Ukumbi wa Diamond Jubilee.
Alhaji Mwinyi alikuwa akizungumzia masuala ya afya na namna ya kujikinga na ugonjwa wa Ukimwi ndipo alipojitokeza mmoja wa waumini aliyekuwa amevalia shati na suruali na kupanda jukwaani kisha kujifanya kama vile anamsalimia Mufti Sheikh Mkuu Issa bin Simba.Kwa kuwa imezoeleka shughuli za kidini kama ile huwa ni za amani basi waliokuwa karibu na mtu huyo wala hawakuwa na shaka naye ndipo mtu huyo akarudisha kibao kwa nguvu na kumzaba Mzee Mwinyi.Mtu huyo alijifanya kama anataka kumsalimia Kaimu Mufti, Sheikh Suleyman Gorogosi.
Kwa kuwa imezoeleka katika shughuli za kidini kutawaliwa na amani, watu waliokuwa karibu na mtu huyo hawakuwa na shaka naye ndipo mtu huyo akarudisha mkono ghafla na kumzaba kibao Mzee Mwinyi.
"Sisi tulishangaa kuona yule jamaa akipanda jukwaani na kujifanya kama anasalimiana na Mufti.
Lakini cha kushangaza tukaona akageuka na kumzaba kibao Mzee Mwinyi... sisi tulishikwa butwaa," alisema Hussein Kauli mmoja ya watu waliohudhuria sherehe hizo. Habari zaidi Soma Mwananchi.
Mi si Muislamu lakini najiuliza kwa muislamu kuslap mzee kama huyu inaswihi?

5 comments:

Anonymous said...

Bado kikwete naye apewe kichapo jukwaani kabla ya 2010

Anonymous said...

Nadhani....wewe uliyeandika....unafikira changa na ujakwneda shule.....

Anonymous said...

...Kwa mujibu wa uislam uzinzi umekatazwa (ni haram) iwe umevaa kondom au hujavaa! Mzee Mwinyi anatumia jukwaa la dini ya kislaam kufundisha watu wazini kwa kutumia kondom, hii ni haramu na amekosea, achilia mbali wanaozini wafe kwa ukimwi, uislam haufuati upepo kwamba sababu mnataka kuzini na mnakufa kwa ukimwi basi uislam uruhusu kuzini kwa kondom. Baya zaidi unaambrisha uovu huo siku ya kuzaliwa yule aliekuja kuukataza uovu huo (Mtume S.A.W). Kwa hiyo Mzee mwinyi alifanya uovu, na kwa mujibu wa Mtume, anasema "ukiona uovu uwondoe kwa mikono yako, au ukemee kwa mdomo au chukia moyoni mwako, ingawa huko kuchukia tu ni imani dhaifu..." Kwa hiyo huyu kijana alomchapa Mzee Mwinyi kibao, machoni mwa wanaadamu ataonekana mtovu wa adabu, muhuni na kila aina ya sifa mbaya, Ila mbele za Allah na waumini wenye kujuwa dini yao, yeye ni shujaa, ni mtu bora na kweli anatafuta radhi za Allah na sio sifa na utukufu wa dunia, kama wengine wanaoacha uislam wao kwa maslahi ya kidunia...!

Anonymous said...

huyu kijana kwa kweli anahitaji pongezi za hali ya juu kwa kufanya kile ambacho kila muislamu au mtu yoyote mwenye fuata maamrisho ya dini yake alitakiwa afanye. kazi aliyoifanya huyu kijana ilitakiwa ifanywe na huyu anayejiita shehe mkuu kwani yeye ndiye anayetakiwa kuhakikisha yaale ambayo allah ametuamrisha na mafunzo ya mtume SAW yanafuatwa. SHEKHE MKUU KWA KWELI ALITAKIWA AWE WA KWANZA KUMCHAPA MZEE MWINYI VIBAO KWA KUTUMIA JUKWAA LA WAISLAMU HASWA HASWA KATIKA SIKU YA KUMKUMBUKA MTUME WETU, KIPENZI CHETU MUHAMMAD SAW ANZALIWA KUAMRISHA WATU WATUMIE KONDOMU MAANA YAKE ANAAMRISHA YALE AMBAYO MTUME NA M'MUNGU AMETUKATAZA. JE? YEYE MZEE MWINYI YUKO TAYARI HAO ANAO WAAMRISHA WATUMIE KONDOMU KUMZINI MAMA YAKE, MKE WAKE, MWANAE, SHANGAZI YAKE AU BIBI YAKE? AU ANAJUA KUSEMA TU? JIBU ATAKALOJIBU ATASEMA HAYUKO TAYARI. HIVYO NDIO MAANA ALLAH NA MTUME WAKE WALITUAMRISHA KUTOKUIKARIBIA ZINAAA. HIVYO MZEE MWINYI ALISTAHILI KUPIGWA SI KIBAO KIMOJA TU BALI ZAIDI YA MILIONI ALIPASWA APIGWE KWA KUTAKA KUUPOTOSHA UMMA WA KIISLAMU. SIKU ZOTE MIMI NAJUA MZEE MWINYI SI MUUMINI WA KWELI BALI NI MNAFIKI NA M'MUNGU AMEMUUMBUA. NA KTK UISLAMU AU SHERIA HAKUNA KUSEMA HUYU MZEE AU MTOTO SHRIA NI MSUMENO. ANACHOTAKIWA MZEE MWINYI KWA SASA NI KUTUOMBA WAISLAMU NA WATANZANIA WOTE RADHI KWA KUTAKA DADA ZETU NA MAMA ZETU NA SHANGAZI ZETU WAJE WAZINIWE NA HAO WATUMIAJI WA KONDOMU. KWA UFUPI MZEE MWINYI ALITAKA KUTUPOTOSHA.

Anonymous said...

huyu kijana kwa kweli anahitaji pongezi za hali ya juu kwa kufanya kile ambacho kila muislamu au mtu yoyote mwenye fuata maamrisho ya dini yake alitakiwa afanye. kazi aliyoifanya huyu kijana ilitakiwa ifanywe na huyu anayejiita shehe mkuu kwani yeye ndiye anayetakiwa kuhakikisha yaale ambayo allah ametuamrisha na mafunzo ya mtume SAW yanafuatwa. SHEKHE MKUU KWA KWELI ALITAKIWA AWE WA KWANZA KUMCHAPA MZEE MWINYI VIBAO KWA KUTUMIA JUKWAA LA WAISLAMU HASWA HASWA KATIKA SIKU YA KUMKUMBUKA MTUME WETU, KIPENZI CHETU MUHAMMAD SAW ANZALIWA KUAMRISHA WATU WATUMIE KONDOMU MAANA YAKE ANAAMRISHA YALE AMBAYO MTUME NA M'MUNGU AMETUKATAZA. JE? YEYE MZEE MWINYI YUKO TAYARI HAO ANAO WAAMRISHA WATUMIE KONDOMU KUMZINI MAMA YAKE, MKE WAKE, MWANAE, SHANGAZI YAKE AU BIBI YAKE? AU ANAJUA KUSEMA TU? JIBU ATAKALOJIBU ATASEMA HAYUKO TAYARI. HIVYO NDIO MAANA ALLAH NA MTUME WAKE WALITUAMRISHA KUTOKUIKARIBIA ZINAAA. HIVYO MZEE MWINYI ALISTAHILI KUPIGWA SI KIBAO KIMOJA TU BALI ZAIDI YA MILIONI ALIPASWA APIGWE KWA KUTAKA KUUPOTOSHA UMMA WA KIISLAMU. SIKU ZOTE MIMI NAJUA MZEE MWINYI SI MUUMINI WA KWELI BALI NI MNAFIKI NA M'MUNGU AMEMUUMBUA. NA KTK UISLAMU AU SHERIA HAKUNA KUSEMA HUYU MZEE AU MTOTO SHRIA NI MSUMENO. ANACHOTAKIWA MZEE MWINYI KWA SASA NI KUTUOMBA WAISLAMU NA WATANZANIA WOTE RADHI KWA KUTAKA DADA ZETU NA MAMA ZETU NA SHANGAZI ZETU WAJE WAZINIWE NA HAO WATUMIAJI WA KONDOMU. KWA UFUPI MZEE MWINYI ALITAKA KUTUPOTOSHA.