Friday, May 08, 2009

POLISI NA MAJAMBAZI DAR




Kimbembe cha majambazi na polisi kurushiana risasi kimemalizika huku polisi wakiwa wameibuka kidedea.
Mchezo huo ulikuwa kama sinema na ulidumu kwa zaidi ya dakika 40 huku shaba zikirushwa kutoka kila upande na damu zilimwagika.
Kila askari alikuwa na bunduki, bastola ama cha kufyatulia mabomu ya machozi. Wake kwa waume.
Kali zaidi ni mikwara baada ya kuwatia mbaloni, utakimbia!!!! Habari kamili na rasmi baadae.


1 comment:

Anonymous said...

kweli Tanzania sasa hivi tupo juu askari wanapigana na majambazi kwa moyo wao wote na inaonyesha dhahiri ni jinsi gani wanavyoipenda kazi yao .Sasa basi serikali ndio inawakatisha tamaa kwa mfano mdogo tu ,askari ameumia akiwa anatetea taifa lake jamani kweli kweli serikali inashindwa kumpeleka nje ya nchi kutibiwa kwakweli inasikitisha sana .