Saturday, February 14, 2009

MATUMLA ABONDWA

Nyumbani ni nyumbani tu, Cheka akipongezwa na walugulu.
Afande Sele akimpongeza Cheka baada ya Ushindi, hii ni mambo ya Dar mpaka Moro.

Mashambulizi yakiendelea usoni mwa Matumla.


Matumla akiondoka akiwa hoi baada ya kichapo hasa round ya 11 kidogo aanguke.
RC Moro, Said Kalembo akimvika mkanda wa Ushindi Cheka.

BONDIA francis Cheka jana usiku aliendeleza ubabe wake kwenye familia ya Matumla baada ya kumpiga kwa mara ya tatu Rashid Matumla kwa pointi kwenye mchezo uliofanyika katika uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Mchezo huo uliohudhuriwa na mashabiki wengi kutoka sehemu mbali mbali za Tanzania ulishudia mabondia hao wakionyesha ujuzi wa kutumia makonde katika raundi zote 12 za mchezo huo.
Majaji wote watatu walimpa Cheka ushindi wa pointi 19/18 dhidi Matumla aliyeonyesha upinzani mkali kwa bingwa huo wa ICT.
Rashid Matumla kabla ya mpambano huo alisema endapo atapigwa atatangaza kujiuzuru rasmi. SIJUI INAKUWAJE SASA?

No comments: