Friday, February 19, 2010

KESI YA MAWAZIRI


KESI ya kutumia madaraka vibaya na kuisababishia serikali hasara ya zaidi ya Sh 11 bilioni inayowakabili mawaziri wa zamani, Basil Mramba, Daniel Yona na Katibu Mkuu mstaafu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Gray Mgonja, itaendelea kunguruma tena mfululizo kuanzia Machi 8 hadi 9, mwaka huu.
Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Anisseta Wambura aliyaeleza hayo jana mara baada ya Wakili wa Serikali, Shadrack Kimaro, kudai kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa na kwamba tarehe za kuendelea kusikilizwa zilikwishapangwa.
Baada ya kutolewa kwa maelezo hayo, hakimu Wambura alisema kesi hiyo itaendelea kusikilizwa Machi 8 hadi 9, mwaka huu na kuamuru washtakiwa wote wawepo siku hiyo.

No comments: