Tuesday, January 04, 2011

CHAMI TO INDIA


Serikali imesema haina ugomvi na mfanyabiashara yeyete kutoka na kuwa wanaruhusiwa kufanya biashara ya aina yeyote isipokuwa wasivunje sheria za nchi.

Akizungumza jijinki Dar es Salaam juzi kabla ya kusafiri kwenda India kwa ziara ya siku saba, waziri wa Viwanda na Biashara, Cyril Chami alisema kuwa kikubwa kwa wafanyabaishara wanaofanya kazi zao nchini ni kufuata taratibu.

“Hata kama wapo wachina na wengine sisi hatuna tatizo nao ili mradi wafuate sheria na taratibu zilizowekwa, vinginevyo hatutaelewana” alisema.

Dk Chami alisema kwa sasa wafanyabishara wengi wamekuwa wakitoka nchi mbalimbali kwajili ya kununua bidhaa mbalimbali nchini na kufanya Dar es Salaam kuwa kama Dubai ya Afrika.

“Wafanyabiashara kutoka Congo, Malawi, Uganda, Zambia nanchi nyingine za jirani wamekuwa wakijazana Kariakoo kwa kjili ya kununua bidhaa mbalimbali hii inaonyesha jinsi biashara inavyokuwa” alisema.

Kutokana na hilo Waziri Chami alisemakuwa atatumia fursa hiyo kushawishi wafanyabaishara wa India na wawekezaji wengine waje kufuwekeza nchini kwani soko tayari limeshakuwa likiwemo la Tanzania na nchi za jirani.

No comments: