Wednesday, March 09, 2011

JERRY AZIDI KUELEMEWA



JERRY Muro na wenzake Edmund Kapama na Deogratias Mgasa wamepatikana na kesi ya kujibu katika mashtaka matatu yanayowakabili likiwemo la kuomba rushwa ya Sh 10 milioni kutoka kwa Mhasibu wa Halmashauri ya Bagamoyo, Michael Kalori.

Mashtaka mengine yanayowakabili washtakiwa hao ni kula njama, na kujitambulisha kuwa wao ni maofisa wa serikali.

Uamuzi huo, ulitolewa jana na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu jijini Dar es Salaam, Gabriel Mirumbe Mara baada ya Wakili wa Serikali Mkuu, Boniface Stanslaus kufunga ushahidi wao wa upande wa mashtaka.

No comments: