Wednesday, March 09, 2011

MWALIKO WA MAANDAMANO KUPINGA UWEPO WA MGODI NZEGA!


Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Nzega inakualika kwenye Maandamano ya Amani kupinga uwepo wa Mgodi wa Kuchimba dhahabu wa Golden Pride Project, Nzega, kwa kuwa hauna faida kwa Nzega na kwa Taifa, Unaharibu mazingira, Umegubikwa na usiri mkubwa, Wachimbaji wadogo na wakazi wa maeneo mgodi huu ulipo hawajalipwa fidia mpaka leo, wananchi wa Nzega hawapati fursa za ajira wala tenda mbalimbali mgodini humo, unatumia maji mengi zaidi ya wenyeji, unachafua na kuharibu vyanzo vya maji, uongozi na wamiliki wa mgodi hawana ubinadamu na huruma kwa wenyeji wa Nzega na hata nchi yetu kwa ujumla n.k.



Maandamano haya yatafanyika Mnamo Tar 3/4/2011 mjini Nzega. Njia zitakazotumika, mahali pa kuanzia na kumalizia maandamano haya mtatangaziwa baada ya makubaliano na Polisi (W) ya Nzega. Tutazidi kutoa taarifa zaidi.




Nyote mnakaribishwa kuunga mkono jitihada hizi za kudhibiti wizi wa Raslimali za Taifa na uharibifu mkubwa unaofanyika!




Wakatabahu,


Ndg. HK.


--


"Vision is the ability to see the invisible!"


Hamisi A. Kigwangalla, MD, MPH, MBA


P.O.Box 22499,


Dar es salaam.


Tanzania.


Phone No: +255 715 636963


+255 784 636963


No comments: